


| HABARI KWA KIFUPI |
| TANGAZA HAPA |
| Qeene NTE Mchomvu |

| WAJUE WATANGAZAJI WAPO RADIO |
| TANGAZA HAPA |

| MERCY MOSES NA TAARIFA YA HABARI |
| W A P O R A D I O T U M E L E N G A K U K U H A B A R I S H A |
| HABARI KAMILI. TANGA: Jamii za wafugaji imetakiwa kujikita katika uzalishaji wa Gesi kwa kutumia kinyesi kutoka katika mifugo,badala ya kutegemea nishati ya kuni pamoja na mafuta ya taa. Hayo yamesemwa Mjini Tanga na Waziri wa Nishati na madini Mheshimiwa WILLIUM NGELEJA wakati akifungua warsha ya siku mbili ya wadau wa uzalishaji wa Gesi Nchini yakiwamo makampuni binafsi. Aidha amesema kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono ikishirikiana na wawekezaji wa teknolojia hiyo. Mheshimiwa NGELEJA amesema sekta binafsi inanafasi kubwa katika kufikisha teknolojia hii ya gesi vijijini ambayo itapunguza mahitaji ya umeme katika maeneo mengi iwapo nguvu itaelekezwa katika eneo hilo. HABARI ZA KIMATAIFA. RTIBLISI Rais wa GEORGIA, MIKHEIL SAAKASHIVILI amesaini Mkataba wa kukomesha mapigano uliopendekezwa na Ufaransa kwa ajili ya Umoja wa Ulaya na ambao unalenga kumaliza mzozo wa kivita katika eneo linalopigania kujitenga na GEORGIA, la OSSETIA ya Kusini. Mkutano huo umesainiwa wakati wa mkutano kati ya Rais MIKHEIL SAAKASHIVIL na Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani BI CONDOLEEZA RISE katika Mji Mkuu wa Georgia TIBLISI. Akizungumza Juu ya Mkataba huo BI, RISE amesema wakati umewadia sasa kwa Urusi kujiunga na mkataba huo. Aidha RISE ameongeza kusema kuwa mkataba huo unapendekeza kutumwa katika eneo ambalo wanajeshi wa kulinda amani kwa kuanzia na waangalizi wa jumuiya ya usalama na ushirikiano barani ulaya OSCE. JOHANNESBURG Mkutano wa kilele wa siku mbili wa viongozi wa Nchi wanachama wa jumuiya ya maendeleo ya nchi za kusini mwa AFRIKA SADC,umeanza leo Mjini JOHANNESBURG Nchini Afrika ya Kusini ambapo jambo kubwa linalozungumziwa ni mgogoro wa Zimbabwe. Rais ROBERT MUGABE,anashiriki katika Mkutano huo kama rais wa Nchi. Kiongozi wa Chama cha Upinzani Cha Mageuzi ya Kidemokrasia cha MDC, MORGAN TSVANGIRAI na kiongozi wa Chama kilichojitenga na MDC ARTHUR MUTAMBARA wanashiriki kama waangalizi pekee. Katika Mkutano huo ambao RAIS THABO MBEKI wa Afrika ya Kusini atachukua Uwenyekiti wa Jumuiya ya SADC kutoka kwa ZAMBIA, unarajiwa kubugikwa hasa na mazungumzo kati ya ROBERT MUGABE na viongozi wa Upinzani juu ya uundwaji wa Serikali ya Umoja wa Taifa. Rais wa BOTSWANA,IAN KHAMA ambaye hakuutambua Ushindi wa Rais ROBERT MUGABE katika Uchaguzi wa Mwezi juni mwaka huu ameususia Mkutano huo wa mjini Johanesburg BERLIN. Kansela ANGELA MARKEL wa Ujerumani ameikosoa Urusi kutokana na jinso ilivyoshughulikia mzozo wa katika OSSETIA ya kusini. Markel ameitaka Urusi kuondoa majeshi yake kutoka katika ardhi ya GEORGIA kama hatua ya kwanza ya kufikia mkataba wa kudumu wa kusimamisha mapigano. Hata hivyo Rais wa Urusi MEDVEDEV amesema kwamwe haitatokea majimbo ya OSSETIA ya Kusini na AKHIBAZIA kuwa sehemu ya Georgia. MOSCOW. Urusi imeonyesha kukasirishwa na mkataba kati ya Marekani na Poland ambo utairuhusu Marekani kuweka Ulinzi wa Makombora yake Nchini POLAND. Rais wa Urusi, DMITRY MEDVEDEV ameyasema hayo katika Mkutano na waandishi wa habari ambapo amesema kuwa ulinzi huo wa makombora unaikusudia Urusi. Maafisa wa Marekani walikanusha mara kadhaa wakisema mpango huo ni kwaajili ya ulinzi wa Marekani na washirika wake dhidi ya kile walichokitaja nchi za wasiojihehimu. Maafisa wakuu wa POLAND na MAREKANI walisaini Mkataba ambao utairuhusu Marekani kuweka kwenye mwambao wa bahari ya BALTIC mitambo yake 10 ya kunasa na kuteketeza, makaombora kwa upande wake,marekani iliahidi kuisaidia Poland kuimarisha jeshi lake la anga. PARAGUAY Rais Mpya wa PARAGUAY, FERNANDO LUGO amekula kiapo kuwa rais wa Nchi hiyo na hivyo kumaliza kipindi cha miongo sita ya Utawala wa Chama cha KONSEVATIVE cha KOLORADO PARTY. Maelfu ya Raia wa PARAGUAY amesherehekea wakati Askofu huyo wa zamani akikabidhiwa madaraka katika Mji Mkuu wa ASUNCION. Akizungumza kwa kutumia Lugha zote mbili za Kihispania na Guarani, ambayo ni lugha yake ya asili Rais FERNANDO HUGO ameahidi kupambana na rushwa na umaskini. Hata hivyo imeelezwa kuwa ahadi hizo ndizo zilizomsaidia mwanasiasa huyo kupata Ushindi katika Uchaguzi ambao Ulifanyika mwezi Aprili mwaka huu. . MWISHO WA TAARIFA YA HABARI KUTOKA WAPO REDIO 98.0 FM. |





| TANGAZA HAPA |

| TANGAZA HUUDUMA YAKO HAPA |
| TANGAZA HAPA |
